January 29, 2014

VAN DER PLUIJM NA MSAIDIZI WAKE MKWASA, LEO.

Kocha Mkuu wa Yanga, Hans van Der Pluijm amesema upepo mkali na uwanja mbovu wa Mkwakwani ni chanzo cha wao kushindwa kufanya vizuri.


Van Der Pluijm amesema walishindwa kuweka mpira chini kama walivyotarajia kutokana na uwanja kutokuwa katika hali nzuri kwenye upande wa kuchezea.
Lakini bado akasisitiza, walipojaribu kuinua mipira juu, haikuwa ikienda kwa kasi inayotakiwa kutokana na kuwa na upepo mkali.
“Niliwaambia wachezaji kuongeza umakini kwa kuwa upepo pia ulitusumbua na kusababisha mpira kupoteza uelekeo,” alisema van Der Pluijm.
“Bado tuna nafasi ya kujirekebisha, tunaweza tukafanya vizuri zaidi ya hapo, lakini lazima tujipange na kitu kizuri tumepata pointi moja.”

Yanga imeshuka kileleni baada ya kuzidiwa pointi moja na Azam FC yenye 33 sasa baada ya kuishinda Rhino 1-0 na Yanga inabaki na 32 kutokana na sare hiyo ya Mkwakwani.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic