January 27, 2014


Kocha Mkuu wa JKT Oljoro ya Arusha, Hemed Morocco, amesema ameshangazwa kupata sare ya bao 1-1 dhidi ya Coastal Union ya jijini Tanga kwa kuwa timu yake ilistahili kushinda kutokana na kiwango ilichokionyesha.


Coastal walilazimishwa sare hiyo juzi katika mchezo wa Ligi Kuu Bara uliopigwa kwenye uwanja wao wa nyumbani wa Mkwakwani, Tanga.

 Morocco, aliyekuwa kocha mkuu wa Coastal katika mzunguko wa kwanza kabla ya kutimuliwa, alisema katika mchezo huo wa juzi, walikuwa na uwezo wa kuwafunga wapinzani wao hao kwenye uwanja wao wa nyumbani.

“Yaani inashangaza kwa kweli kutoka sare na Coastal kutokana na kiwango tulichokionyesha, tulicheza mpira mzuri zaidi yao na tulikuwa tukifanya mashambulizi ya mara kwa mara langoni mwao, ila nafikiri haikuwa bahati yetu kwa sababu tuliwakamata kwa kiwango kikubwa,” alisema Morocco.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic