February 13, 2014


Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) limeruhusu mshambuliaji Emmanuel Okwi kuichezea Yanga.


Taarifa za uhakika kutoka ndani ya TFF ambazo zimethibistishwa na Katibu Mkuu wa Shirikisho hilo, Mwesigwa Celestine zimesema kuwa Okwi sasa ni huru.
“Kweli hilo tumetaarifiwa lakini tutalizungumzia baadaye,” alisema.
TFF ndiyo ilisimamisha usajili wa Okwi kwa madai ya kutaka ufafanuzi kutokana na kesi tatu za kimsingi kati ya Okwi, Etoile du Sahel.
Sasa Okwi atakuwa huru kuanza kuitumikia Yanga ambayo imesamjili kwa dau la zaidi ya dola 100,000 (Sh milioni 160).

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic