February 4, 2014


Chelsea imeonyesha mpira uko tofauti siku zote na wengi wanavyoamini kwa kuichapa Man City kwa bao 1-0 ikiwa kwao Etihad jijini Manchester.


Bao la Chelsea katika mchezo huo lilifungwa na beki wake wa kulia Branislav Ivanovic ambaye aliukuta mpira unaelea baada ya Ramirez kupiga shuti lililowababatiza mabeki wa Man City, naye akautupia kambani kiufundi utafikiri mshambuliaji.

Katika mechi hiyo ya Ligi Kuu England iliyomalizika punde, kocha Jose Mourinho wa Chelsea ameingia vyumbani haraka hata bila ya kumsalimia Pellegrini hali iliyoonyesha kuwa amechanganyikiwa na furaha ya ushindi wa mechi hiyo.


Pamoja na ushindi huo, Chelsea imeendelea kubaki katika nafasi ya tatu, ikiwa na pointi 53 sawa na Man City lakini tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa yanawabakiza vijana hao wa Manuel Pellegrini katika nafasi ya pili.

Arsenal ambayo jana iliichapa Crystal Palace inabaki katika nafasi ya kwanza ikiwa na pointi 55, hivyo kufanya ushindani kuwa mkubwa zaidi kwa timu tatu hizo ingawa Liverpool yenye pointi 47 si ya kuidharau.



Katika mechi ya leo, Chelsea ndiyo ilipoteza nafasi nyingi huku ikionyesha soka tofauti la kushambulia kwa ‘kaunta atak’ tofauti na wengi walivyotarajia kuwa itapaki basi ili kuzuia kasi ya upigaji mabao ya Man City.
Kama washambuliaji wa Chelsea wangetulia kidogo tu, basi wangekuwa na uwezo wa kufunga hata mabao mengine angalau mawili na kupata ushindi mzuri zaidi ya huo wa 1-0.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic