February 5, 2014





Kocha Mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic, amefunguka kuwa, anahofia kikosi chake kupata majeruhi katika kipindi hiki cha lala salama kwani watamharibia mipango yake.
     

Simba ipo nafasi ya nne ya msimamo wa ligi kuu kufuatia kuwa na pointi 30, nyuma ya Mbeya City yenye pointi 31, ambapo inahitaji kujipanga ili iweze kufanikiwa kusonga mbele.

Loga alisema anahofia majeruhi katika kikosi chake kwani wanaweza kusababisha kutokuwa na kikosi kizuri kwa kuwa kila mchezaji anamtumia kulingana na mfumo.
 “Ligi ni ngumu na hakuna timu kubwa wala ndogo katika kipindi hiki kwani kila timu imejiandaa vya kutosha, hivyo tunahitaji kujipanga pindi tunapokutana na timu yoyote.
“Kitu kikubwa kinachonipa hofu ni kuhusu majeraha kwa wachezaji kwani yatasababisha kutokuwa na kikosi bora.

“Kwa sasa sina kikosi cha kwanza na ninatumia mchezaji kulingana na mechi kwani kuna baadhi wanajua mfumo huu na wengine wanajua mfumo mwingine, hivyo wote wapo sawa.
“Wachezaji ambao ni majeruhi kwa sasa ni Said Nassoro ‘Chollo’ ambapo Donald Musoti alikuwa anasumbuliwa na malaria, pia kuna baadhi ya wachezaji wanacheza huku wakisumbuliwa na majeraha madogo-madogo,” alisema Loga.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic