February 5, 2014



 
MWAMBUSI (KUSHOTO) AKIWA NA MSAIDIZI WAKE
Kocha wa Mbeya City, Juma Mwambusi, amefunguka kuwa wanasahau kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa Yanga, lakini hawatapoteza pointi dhidi ya Simba na Mtibwa Sugar.
 
Mbeya City inatarajiwa kucheza na Simba na Mtibwa kati ya tarehe 9 na 15 katika Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya, uwanja ambao wamekuwa wakipata matokeo mazuri.

Katika mchezo wa kwanza dhidi ya Simba kwenye Uwanja wa Taifa, vijana hao walifanikiwa kupata sare ya mabao 2-2.

 Mwambusi amesema wanasahau kipigo hicho, badala yake wanajiandaa dhidi ya Mtibwa ambayo watakutana nayo wikiendi ijayo na baadaye watawasubiri Simba.

“Kitu kikubwa kilichotufanya tufungwe na Yanga ni kutokana na mwamuzi kuwavuruga wachezaji wangu kisaikolojia.

“Kitendo cha kumpa mchezaji wetu muhimu kadi nyekundu kilivuruga kabisa timu yangu baada ya kutulazimisha kubadili mfumo mzima.
 “Tunajiandaa kuweza kushinda katika uwanja wa nyumbani ambapo nitatumia muda huu wa wiki moja kuweza kukiimarisha kikosi changu ili tuweze kusonga mbele.

“Tunaamini kuwa Mtibwa Sugar na Simba ambazo zinakuja kwetu hazitatoka na pointi.

“Baada ya mechi nne mbele ndiyo nitajua nafasi ya timu yangu itakuwa wapi ukiachana na hii ya Yanga ambayo tumekutana nayo leo,” alisema Mwambusi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic