February 19, 2014



Kocha Mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic amesema kuitoa Simba kwenye mbio za ubingwa msimu huu ni kosa kubwa.

Logarusic amesema Simba bado ina nafasi ya kufanya vizuri kwa kuwa ligi bado mbichi na si kama wengi wanavyoamini.
“Sare yetu na Mbeya City haiwezi kuwa imetutoa kwenye kuwania ubingwa. Bado tunapambana na tunataka kufanya vizuri,” alisema.
Logarusic alisema Simba ni kati ya timu zenye kikosi kizuri na chenye wachezaji wenye uwezo hivyo hawana sababu ya kuhofia.
“Ushindani kwenye ligi leo unaiangusha Simba, kesho timu nyingine. Lakini sisi bado hatujateteleka hata kidogo,” alisema.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic