February 5, 2014





Kocha Mkuu wa Azam FC, Mcameroon, Joseph Omog, amesema kikosi chake kipo kamili kwa ajili ya michuano ya Kombe la Shirikisho.


Azam itaingia kwenye Uwanja wa Chamazi jijini Dar es Salaam keshokutwa Jumapili kuvaana na  Ferroviario de Beira ya Msumbiji katika mchezo wa awali.

Kocha huyo alisema kuwa katika michezo ya ligi kuu, amepata changamoto nyingi sana ambazo zinampa nafasi ya kuweza kuendelea kukiboresha kiwango cha timu yake.

Alisema kwa sasa anaendelea kuangalia kikosi chake kupitia ule upungufu alioweza kuubaini kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wao wa Jumapili.

“Nimepata matumaini makubwa sana kupitia mechi za ligi kuu katika viwango vya wachezaji wangu, hasa kuelekea michuano ya Kombe la Shirikisho tunayojiandaa nayo kwa sasa, japo muda umebaki mchache sana.

“Naamini wapinzani wetu wa huko Msumbuji ni wazuri  japo siwafahamu na sijawahi kuwaona lakini timu yangu bado naamini itafanya vyema kwa jinsi  watakavyofuata kile  ninachokifundisha na wakakielewa,” alisema Omog.

Azam imepata nafasi hii baada ya kushika nafasi ya pili kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara msimu uliopita.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic