February 3, 2014

MGOSI WAKATI AKIKIPIGA SIMBA

Mshambuliaji wa Mtibwa Sugar, Mussa Hassan Mgossi, anataka kuiadhibu timu yake ya zamani, Simba kwa kuhakikisha Mtibwa inachukua pointi tatu keshokutwa Jumatano katika mchezo wa Ligi Kuu Bara kati yao kwenye Uwanja wa Jamhuri, Moro.


Mgosi aliichezea Simba kwa mafanikio makubwa na alikuwa mfungaji bora wa Ligi Kuu Bara msimu wa 2009/2010 wakati Wekundu wakitwaa ubingwa. Keshokutwa ataivaa timu yake hiyo ya zamani akitaka pointi tatu muhimu.

Mgosi amesema ligi ni ngumu nakwa upande wao, baada ya kufungwa na Azam na kutoka suluhu na Kagera, wanataka kuonja ushindi wa kwanza wa mzunguko wa pili dhidi ya Simba.


 “Ligi ni ngumu, kuna ushindani wa hali ya juu na tunahitaji kushinda mchezo wetu, nimejiandaa vyema ili kuweza kufunga katika mchezo huo, lengo letu ni kuhakikisha tunaisaidia timu yetu ili iweze kufanikiwa kumaliza katika nafasi nzuri,” alisema Mgosi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic