February 5, 2014





Kocha Mkuu wa Ashanti United, Abdallah Kibadeni, amezitaja wazi mechi rahisi kwake zilizobaki kwenye mzunguko wa pili wa ligi zinazoweza kumpa ushindi ambazo ni dhidi ya Simba SC, Azam FC na Coastal Union.
 
Kibadeni alisema kuwa anapokutana na timu hizo inakuwa rahisi zaidi kuwa na matumaini ya ushindi kutokana na timu hizo kucheza kwa kujiamini zaidi.

“Unajua mechi ambazo zinaweza kutupa ushindi ni zile tutakazokutana na Simba, Azam au Coastal, Yanga alikuwemo kwenye kundi hili lakini kwa bahati mbaya tulipoteza kwenye ule mchezo tuliokutana nao.

“Timu hizi nne nilizokutajia mechi zake huwa nyepesi kuliko hizi nyingine zilizobaki ila watu huwa hawajui tu, unapokutana nao mchezo huwa rahisi, hawakamii mechi na hucheza kiufundi zaidi, kitu ambacho ni tofauti na unapokutana na hawa wengine kwa sababu hukamia na kufanya mambo yawe magumu zaidi.
“Angalia tulipocheza na Yanga tukafungwa 2-1, tulicheza vizuri kuliko mechi ya Mgambo tuliyofungwa 2-0 ambapo mpira haukuwa mzuri kutokana na timu pinzani kukamia zaidi.

“Timu kubwa zinacheza kwa kujiamini zaidi lakini hizi ndogo ni matatizo, kupata pointi kwao ni kazi ngumu sana,” alisema Kibadeni.
 Aidha, Kibadeni aliongeza kwa kusema hizi timu nyingine zinapotaka kushuka daraja ndiyo huamua kufanya hivyo ili zipate wa kushuka naye lakini Azam, Coastal, Simba na Yanga hazina sababu ya kufanya hivyo kwa kuwa zenyewe huangalia zicheze vipi kiufundi ziweze kutwaa ubingwa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic