February 5, 2014



Timu ya soka ya Mtibwa Sugar imesema imejipanga kikamilifu kuikabili Simba na kwamba wasitegemee ushindi.


Simba inavaana na Mtibwa leo, Jumatano kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro katika mchezo mkali wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara.

Meneja wa timu hiyo, David Gboya, alisema timu ya Simba ni nzuri lakini hata wao wana timu nzuri na mwisho wa siku wanategemea ushindi.

"Siyo kwamba tunacheza na Simba ndiyo twende kinyonge bali tunaenda kupambana ili tuibuke na ushindi ukizingatia tumepoteza mchezo wetu wa kwanza dhidi ya Azam na wa pili tumetoka sare dhidi ya Kagera.

“Tunaamini kuwa tuna uwezo wa hali ya juu wa kuibuka na ushindi kwa kuwa tumejiandaa vyema na hatuna hofu yoyote hadi sasa,” alisema Gboya.

Mchezo huo unatarajiwa kuwa mkali na wa kusisimua na Simba wanafahamu kuwa ushindi tu ndiyo utafufua matumaini yao ya kutwaa ubingwa msimu huu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic