February 5, 2014





Straika wa Simba, Amissi Tambwe, amesema mpira wake aliopewa baada ya kufunga mabao matatu ‘hat trick’ katika mchezo  dhidi ya Oljoro ni kumbukumbu ya kipekee kwake na ameahidi kuupeleka kuutunza kwao Burundi kama kumbukumbu.
 
Tambwe, alipiga hat trick, Jumamosi iliyopita wakati timu yake ikiwasambaratisha maafande wa JKT Oljoro kwa mabao 4-0, bao lingine likiwekwa kimiani na Jonas Mkude.

Nyota huyo wa zamani wa Vital ‘O ya Burundi, alisema ataupeleka kwao ili mke wake na mtoto wawe wamkumbuke kupitia mpira huo na kuthamini kazi yake huku Tanzania.

“Ilikuwa ni mara ya kwanza kupewa haki yangu kihalali, kwangu ni kumbukumbu na ninataka mke na mtoto wangu Flory kila watakapouangalia wanikumbuke na kuthamini ninachofanya huku Tanzania,” alisema Tambwe.

Hat trick hiyo ni ya pili kwake baada ya mabao manne aliyofunga dhidi ya Mgambo Shooting katika ushindi wa mabao 6-0 raundi ya kwanza, lakini hakupewa haki yake baada ya mchezo.

Aliongeza kuwa iwapo atafanikiwa kufunga hat trick nyingine iwe kwenye mchezo wa leo dhidi ya Mtibwa au siku nyingine, mpira huo atautoa kama zawadi kwa marehemu mama yake.

“Huu siwezi kuutoa kama ‘dedication’ (zawadi), ni kumbukumbu muhimu kwangu, mara ya kwanza walininyima haki yangu, lakini iwapo nitabahatika kufunga tena, hiyo itakuwa ni zawadi kwa mama yangu. Nilimpenda sana, najua bila yeye nisingekuwa hapa wala kuwa na mafanikio haya, bahati mbaya hayupo duniani,” aliongea kwa unyonge.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic