February 20, 2014


Mashabiki wa Simba waliokuwa wamekwenda mjini Mbeya kuishangilia timu yao katika mechi ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Mbeya City, wamelalama.

Wakizungumza na blog hii, mashabiki hao wamesema Mbeya City walifanya vitendo vingi vya kuiungwana ikiwa ni pamoja na kumchania jezi shabiki mmoja wa Simba.
“Hata sisi Simba na Yanga, kuna ugomvi uwanjani tu hasa shabiki anapokwenda kukaa upande ambao si sahihi.
“Lakini Mbeya City walikuwa wakifanya unyama huo mitaani, walimrukia na kumchania jezi mwanachama wa Simba.
“Sasa timu gani inataka kucheza bila ya wapinzani, tatizo ni lipi mtu kuvaa jezi yake. Kweli hawakuwa sahihi,” alisema Ngade.
“Nafikiri kuna kila sababu walifanyie kazi hilo, maana walipokuja hapa Dar utaona hakuna mtu aliyewafanyia vurugu.”
Katika mechi hiyo, Simba na Mbeya City zilimaliza mchezo kwa sare ya bao 1-1.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic