March 26, 2014





Baada ya timu ya soka ya Ndanda ya mkoani Mtwara kufanikiwa kupanda daraja hadi LIgi Kuu Bara, sasa wachezaji wa timu hiyo wataondoka Dar es Salaan keshokutwa Ijumaa na kurudi mkoani humo kwa usafiri wa ndege wa Shirika la Tanzania (ATC).
 
Hiyo itakuwa ni mara ya kwanza kwa wachezaji wa Ndanda kusafari kwa ndege tangu ilipoanzishwa Mach 28, 2011 katika kijiji cha Ndanda kilichopo wilayani Masasi.
Katibu Mkuu wa Ndanda, Selemani Kachele aliliambia Championi Jumatano kuwa baada mkuu wa mkoa wa Mtwara, Joseph Simbakalia, kupata taarifa za timu hiyo kupanda daraja aliamua kutoa ofa hiyo kwa wachezaji pamoja na viongozi wote wa kikosi  hicho.
Alisema kuwa, Simbakalia amefanya hivyo kama moja ya shukrani zake kwa wachezaji pamoja na viongozi kwa jitihada zao walizozionyesha kwenye michuano hiyo ya Ligi Daraja la Kwanza na kufanikiwa kupanda daraja mpaka Ligi Kuu Bara.

“Mbali na hilo pia ametuandalia sherehe kubwa ambayo itaambatana na mapokezi ya aina yake mara tu tutakapotua mjini Mtwara siku hiyo ya Ijumaa.

“Hakika tunamshukuru kwa mchango wake huo na tunawaomba wananchi wa Mtwara kujitokeza kwa wingi siku hiyo kwa lengo la kuwapokea vijana wao waliopigana kwa nguvu zote na kurudisha heshima ya mkoa wetu iliyokuwa imepotea kwa miaka 10 tangu Bandari iliposhuka daraja,” alisema Kachele .

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic