March 26, 2014





Mshambuliaji nyota wa Yanga, Emmanuel Okwi amesema kila inapofika usiku amekuwa akitumia muda wake kutafakari kuhusiana na mabao.


Ameiambia SALEHJEMBE kwamba, mara kadhaa kila
anapokuwa ametulia usiku amekuwa akijiuliza namna ya kufanya kuhakikisha anafunga katika mechi ya leo dhidi ya Prisons ya Mbeya.

“Hata kama nikishindwa kufunga, basi angalau nitoe hata pasi tatu za mabao. Natamani tuendelee kushinda kama ilivyokuwa Tabora.
“Lakini pia ninataka kufunga, kwa mchezaji kufunga bao kwa ajili ya timu yako ni jambo jema sana. Lakini sisemi ni lazima, kama ikiwa ni sehemu ya kutoa pasi, nitafanya hivyo mara moja,” alisema Okwi.
Mganda huyo aliyewahi kukipiga Simba, amekaukiwa mabao baada ya kuichezea Yanga mechi tano na kufunga bao moja tu.
Lakini amekuwa chachu ya pasi za mabao ya Yanga na pia msumbufu kwa mabeki wa timu pinzani.
Okwi anasifika kwa kasi na chenga za maudhi, lakini akipata nafasi amekuwa akifunga kwa mashuti makali.
Okwi amewahi kukipiga Simba na kujenga jina kubwa nchini kabla ya kuondoka na kwenda kujiunga na Etoile du Sahel ya Tunisia.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic