March 15, 2014


Kocha Msaidizi wa Yanga, Boniface Mkwasa, amesema kikosi ni bora na kina uwezo wa kuifunga timu yoyote hapa nyumbani kama maelekezo yakifuatwa kwa uhakika.

Lakini akasema mechi yao ya leo mjini Morogoro dhidi ya Mtibwa Sugar itakuwa ngumu kutokana na kiwango duni cha uwanja huo.
“Bado uwanja si mzuri sana, ndiyo maana ninaweza kusema kutakuwa na ugumu katika mechi hiyo,” alisema Mkwasa.

“Utaona tofauti ya Yanga inapokuwa inacheza kwenye uwanja duni na uwanja bora kama ule wa taifa, bado tuna matatizo ya viwanja,” alisema Mkwasa.

Mechi hiyo ya Ligi Kuu Bara itakuwa ni ya kwanza kwa Yanga tokea irejee nchini ikitokea Misri ilipokwenda kukipiga na Al Ahly ambayo iliwang’oa mabingwa hao wa Tanzania Bara katika Ligi ya Mabingwa Afrika.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic