March 25, 2014


Mshambuliaji wa Yanga, Emmanuel Okwi amesema anataka kufunga lakini mambo hayakai sawa.

Jambo hilo limekuwa likimpa wakati mgumu na amepania kupata mabao katika mechi zinazofuata za Yanga.
Akizunguma na SALEHJEMBE, Okwi amesema ingawa anatakiwa kutengeneza nafasi za mabao kama ambavyo amekuwa akifanya, lakini anatamani kufunga.
“Zaidi ya mechi mbili sasa, sijisikii vibaya lakini nataka kufunga mabao na kuisaidia timu yangu.
“Ninajua nina uwezo huo, lakini mambo huwa yanakataa wakati fulani.
“Mechi zijazo tutashirikiana zaidi na ninaamini ninaweza nikafunga au kutengeneza nafasi zaidi,” alisema.

Mganda huyo amekuwa akitengeneza nafasi nyingi zaidi za mabao katika kikosi cha Yanga, lakini Yanga imekuwa na tatizo la kupoteza nafasi hizo za kufunga.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic