March 24, 2014

 
MESSI AKIITUMIKIA SIMBA KATIKA MOJA YA MECHI ZA LIGI KUU BARA
Kiungo mshambuliaji wa Simba, Ramadhani Singano ‘Messi’ amevunja vioo vya mlango wa uwanja wa Taifa mara tu baada ya mechi yao dhidi ya Coasal Union kumalizika.

Katika mechi hiyo, Simba walilala kwa bao 1-0 na Messi alipoteza nafasi safi katika dakika ya 90 baada ya kubaki yeye na kipa lakini akashindwa kufunga.
Hali hiyo ilionyesha kumchanganya na wakati anaingia vyumbani aliupiga teke mlango na kuvunja vioo.
Kutokana na hali hiyo, askari waliingia na kutaka mumtia nguvuni, lakini Katibu Mkuu wa Simba, Ezekiel Kamwaga alijitokeza na kuanza kuzungumza nao.
Baada ya mazungumzo hayo ya dakika kadhaa wakiwa na Kamwaga, askari walionyesha kuiiondoa katika jambo hilo.

Mmoja wa askari hao alisema wameliacha jambo hilo mikononi mwa Simba na uongozi wa uwanja wa Taifa na kitu kizuri kwao, aliyevunja mlango huo anajuikana.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic