March 3, 2014


Mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Ben Mwalala, amewataka Yanga kujipanga vizuri kwa ajili ya mechi ya marudiano dhidi ya Al Ahly itakayopigwa nchini Misri Jumapili ijayo.


Mwalala ameliambia gazeti hili kuwa, ili Yanga waweze kufanya vizuri katika mechi hiyo, wachezaji wote wanatakiwa kucheza kwa nguvu bila ya kutegeana kuanzia dakika ya kwanza hadi ya mwisho.
Alisema katika mechi ya juzi iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar, kuna baadhi ya wachezaji walikuwa hawatekelezi majukumu yao ipaavyo, ndiyo maana kuna wakati Al Ahly walionekana kutawala mchezo huo.
“Waliokuwa wanapambana muda wote walikuwa ni Frank Domayo, pamoja na safu ya ulinzi, hao walikuwa wanakaba mwanzo mwisho lakini wengi waliobakia walikuwa hawafanyi majukumu yao kama inavyotakiwa.

“Hivyo basi katika mechi ya marudiano watu wote wanatakiwa kupambana na kukaba kwa nguvu ili kuhakikisha wanaibuka na ushindi kwenye mechi hiyo,” alisema Mwalala ambaye alikuwepo katika kikosi cha Yanga kilichochapwa jumla ya mabao 4-0 na Al Ahly mwaka 2009, Dar wakipigwa moja na ugenini 3-0.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic