March 3, 2014


Shabiki wa Yanga aliyefahamika kwa jina la Joseph William, mkazi wa Gongo la Mboto, Dar es Saalam, alipasuliwa paji la uso na mashabiki wenzake uwanjani, hali iliyosababisha ashonwe nyuzi zaidi ya 12 huku mwenzake mmoja, Hamza Abdallah wa Ilala, akichanwa pembeni ya uso baada ya kupigwa na nati za kufungia viti.

Matukio hayo yalitokea juzi katika mchezo wa Yanga dhidi ya Al Alhy uliochezwa  Uwanja wa Taifa jijini Dar na Yanga kuibuka na ushindi wa 1-0.
Mashabiki hao walipata majeraha baada ya kuwa wanagombana uwanjani kwa kutupiana viti wakati mechi ikiendelea lakini hali zao zinaendelea vizuri.

Mashabiki hao wa Yanga walikuwa wakitupiana viti na mashabiki wanaodaiwa ni wa Simba waliokuwa wanaisapoti Al Ahly.
Akizungumza na Championi Jumatatu, mmoja madaktari wa huduma ya kwanza uwanjani hapo, aliyefahamika kwa jina moja la Nassor, alisema majeruhi hao walipata matibabu  hapo.

“Mashabiki hawa wawili ndiyo tuliowapokea na wote ni wa Yanga, wamepata majeraha baada ya kutupiwa viti pale uwanjani wakati mchezo ukiendelea, Joseph William wa Gongo la Mboto kashonwa nyuzi zaidi ya 12,” alisema daktari huyo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic