March 3, 2014


Baadhi ya kiungo wa Yanga, Frank Domayo ‘Chumvi’ kuonyesha kiwango kizuri na kupiga pasi nyingi za uhakika katika mchezo wa juzi Jumamosi wa kimataifa dhidi ya Al Ahly, benchi la ufundi la Waarabu hao limeonekana kumtamani.


Kocha Msaidizi wa Al Ahly ambao ndiyo mabingwa watetezi wa michuano hiyo ya Ligi ya Mabingwa Afrika, El Sayed Abdelhariz, amesema Domayo anastahili kuwa miongoni mwa wachezaji wa timu yake.

 Abdelhariz alisema Domoyo ndiye mchezaji aliyeharibu mipango yao katika mechi hiyo iliyokuwa na ushindani mkubwa.
“Tumeyapokea matokea hayo na tunarudi nyumbani kujipanga kwa ajili ya mechi ya marudiano japokuwa kuna mambo mengi yaliochangia tukafungwa, kama vile hali ya hewa ambayo ilikuwa ikiwasumbua sana wachezaji wetu.
“Mipango yetu ilikuwa ni kushinda lakini mambo yamekuwa tofauti na tulivyotarajia, hata hivyo katika mchezo huo, mchezaji aliyetusumbua zaidi alikuwa yule aliyekuwa amevaa jezi namba 18 (Domayo), kwani alikuwa anaharibu mipango yetu kila wakati kutokana na uwezo wake mkubwa wa kukaba na kuanzisha mashambulizi makali kwa kupiga pasi za uhakika, anastahili kuwa miongoni mwa wachezaji wa kikosi chetu,” alisema  Abdelhariz.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic