March 24, 2014





Kocha Mkuu wa Azam FC, Joseph Omog, amesema amekuwa akishindwa kulala vizuri kutokana na kufikiria kuchota pointi 15 katika michezo yote mitano iliyobaki ili kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara.


Baada ya mchezo wa jana Jumapili dhidi ya JKT Oljoro kwenye Uwanja wa Chamazi jijini Dar, Azam imebakiza michezo mitano tu dhidi ya Mgambo, Simba, Ruvu,  Mbeya City na JKT Ruvu.


Omog amesema bado ana kibarua kigumu cha kuchukua ubingwa wa ligi hiyo kutokana na kuwa na upinzani mkali kutoka kwa Yanga na Mbeya City.

Omog amesema ni vigumu kujihakikishia nafasi ya ubingwa katika kipindi hiki kwa kuwa kuna mechi nyingi ngumu ambazo itabidi akabiliane nazo.
“Mechi sita zilizobakia ni nyingi sana, hivyo siwezi kusema kama nitachukua ubingwa wa ligi kwa kuwa, kila timu inajipanga ili ishinde, tutajipanga kufanya vizuri katika michezo inayofuata ili tujiweke katika mazingira mazuri.
“Matokeo ya leo ni mazuri na wachezaji wameonyesha kiwango, tunahitaji kuimarika zaidi ili tufanye vizuri,” alisema Omog.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic