March 3, 2014


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadick, ameitabiria makubwa timu ya Yanga kuwa itawafunga tena Al Ahly ya Misri kwenye mechi yao ya marudiano.

Yanga juzi ilishinda kwa bao 1-0 huku ikitarajia kurudiana na wababe hao baada ya wiki moja huko Cairo, Misri.

Sadick alikuwa mmoja wa viongozi waliohudhuria mtanange huo ambapo alisema amefurahishwa na kiwango kilichoonyeshwa na wachezaji wa Yanga ambacho kinampa moyo kuwa Yanga itafanya vizuri kwenye mchezo wa marudiano.

Alisema kuwa ameiona Ahly kuwa haina nguvu, wazito na mwisho kabisa si wajanja wa kuweza kuifunga kwa wepesi hata kama wakiwa kwao, hivyo hana tatizo juu ya Yanga kwenye mechi yao hiyo inayotarajiwa kuwa ngumu.
“Wale hawatuwezi, tuliwazidi kila sehemu, mpira wote tumecheza sisi, hawana stamina, halafu si wajanja wa kuweza kuwazidi wachezaji wa Yanga, tutawafunga tena huko kwao wala tusiwe na wasiwasi,” alisema Sadick.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic