April 19, 2014


Mabingwa wapya wa Tanzania, Azam FC, wamekabidhiwa rasmi kombe lao na Rais wa TFF, Jamal Malinzi.
Kombe hilo limekabidhiwa baada ya Azam FC kukipiga na JKT Ruvu na kuichapa timu hiyo ya jeshi kwa mabao 1-0 ambayo imeteremka daraja.
Bryan Umonyi, raia wa Uganda ndiye alifunga bao hilo baada ya kuingia kuchukua nafasi ya Kipre Tchetche.
Hadi wanakabidhiwa kombe, mechi hiyo ilikuwa imejaza watu wengi na mashabiki wakiwa wengi kwa kuwa pambano hilo halikuwa na kiingilio.

Lakini pia kulikuwa na shoo kutoka kwa vikundi mbalimbali wakiwemo Wanaume TMK walioongozwa na Mheshimiwa Temba.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic