April 19, 2014


Kipa namba moja wa Simba, Ivo Mapunda, amesema wamejipanga vyema kuhakikisha wanaifunga Yanga katika mchezo wa leo.

Yanga na Simba zinatarajiwa kukutana leo Jumamosi katika Dimba la Taifa jijini Dar es Salaam kwenye mchezo wa hitimisho la msimu wa ligi kuu 2013/2014.

Mchezo huo wa watani wa jadi unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa ikiwa kila upande ukihitaji kujenga heshima.

Ivo ambaye ni kipa wa zamani wa Yanga, alisema wanahitaji kufanya maandalizi ya kufa mtu ili waweze kushinda mchezo huo.

“Kushinda na kushindwa ni matokeo ya mpira kwani mpira ni dakika 90, lolote linaweza kutokea lakini sisi tumejipanga kuhakikisha tunamfunga mpinzani wetu kwa lengo la kulinda heshima yetu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic