April 26, 2014

KAVUMBAGU (MWENYE KOFIA KATIKATI) AKIWA KATIKA KIKOSI CHA YANGA KILIPOWASILI JIJINI CAIRO

Mshambuliaji Didier Kavumbagu wa Yanga, kwa mara ya kwanza amefunguka kuhusiana na timu hiyo kukosa ubingwa katika hatua za mwisho.

Kavumbagu ameiambia SALEHJEMBE kuwa, kushindwa kuitoa Al Ahly kulishusha ari ya wachezaji wa Yanga na kusababisha wengi kucheza chini ya kiwango.
Mshambuliaji huyo mrefu na mwenye purukushani nyingi amesema Yanga ilianza kupotea baada ya kurejea kutoka Misri.
“Tuliona kuwa tulistahili kabisa kuitoa Al Ahly, baada ya kushindwa ilimuumiza sana kila mtu. Hivyo tuliporejea kwenye ligi, mambo hayakuwa mazuri.
“Utaona tulishindwa kufanya vizuri, tukaanza kutoka sare mechi tulizotakiwa kushinda.
WACHEZAJI WA YANGA WAKIWA KWENYE BENCHI BAADA YA KUPOTEZA MECHI DHIDI AL AHLY JIJINI ALEXANDRIA.

“Lakini mambo yakawa mabaya zaidi kwa sababu tulifikia hadi kupoteza kwa Mgambo kule Tanga. Hapo ndiyo tulipotea na kuwapa Azam nafasi ya kutwaa ubingwa.
“Lakini hauwezi kusema Yanga ilikuwa na kikosi kibaya, ina kikosi kizuri na kinaweza kushinda dhidi ya timu yoyote ile,” alisema.
Katika mechi mbili za Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Al Ahly ya Misri, Yanga ilianza kwa kuifunga timu hiyo bao 1-0 jijini Dar ingawa ilistahili kushinda.

Ikapoteza kwa idadi hiyo ya bao 1-0 mjini Alexandria, mechi ikaenda katika mikwaju ya penalti bado Yanga ikapoteza licha ya kwamba ilikuwa na nafasi zaidi ya wenyeji kusonga mbele.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic