April 28, 2014





Beki wa kati wa Simba na timu ya taifa ya Burundi, Gilbert Kaze, ameweka bayana kuwa, anawasubiri Simba wampe chake aende kwao akapumzike.

Licha ya uongozi wa Simba kutotaka kuweka wazi hatma ya beki huyo msimu ujao, lakini taarifa chini ya kapeti zinasema nyota huyo ameonyeshwa mlango wa kutokea kwa kile kilichodaiwa ni kiwango kidogo pamoja na kuwa nje kwa muda mrefu akisumbuliwa na jeraha la goti.
Kaze alikiri kusikia taarifa hizo na kusema kuwa anawasubiri Simba wamkatie chake ili atimke na kuongeza kuwa hawezi kucheza tena Tanzania baada ya kutemwa Simba.
“Nasikia taarifa kama hizo na kama zina ukweli, sawa, mimi nasubiri Simba wanipe fedha zangu, maana nina mkataba wa mwaka na nusu mbeleni, nilisaini miaka miwili na nusu. Kwa hiyo kama wameamua kuniweka pembeni poa tu.
“Lakini ukweli ni kwamba siwezi kubaki Tanzania iwapo nitaondoka Simba, nitakwenda nyumbani ili nijitibu goti kisha nitaangalia timu hukohuko, ila siyo hapa Tanzania,” alisema beki huyo aliyeiokoa Simba kutofungwa na Yanga msimu huu, kwa bao lake la dakika 84 lililoipa sare ya mabao 3-3.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic