Michuano ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa
(RCL) itakayochezwa kwa ligi ya mkondo mmoja katika vituo vitatu vya timu tisa
kila kimoja inatarajia kuanza Mei 10 mwaka huu.
Timu ya kwanza kutoka katika kila
kituo ndiyo itakayopanda daraja kucheza Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu wa
2014/2015. Kwa vile ligi hii haina mdhamini, hivyo timu zitajigharamia kwa kila
kitu.
Vituo vitakavyotumika kwa ajili ya
RCL, kanuni pamoja na ratiba vitatangazwa kabla ya kuanza kwa ligi hiyo. Pia
kituo kitakachoteuliwa kwa ajili ya ligi hiyo, timu yake haitapangwa katika
kituo husika ikiwa ni moja ya njia ya kuhakikisha kanuni ya mchezo wa kiungwana
(fair play) inazingatiwa.
0 COMMENTS:
Post a Comment