April 21, 2014





Kocha Mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic, amesema ili kikosi cha Simba kiwe bora msimu ujao, ni vyema wakasajiliwa wachezaji wenye viwango vya hali ya juu ili kurudisha heshima ya timu.


Simba imemaliza ligi ikiwa katika nafasi ya nne ikiwa na pointi 38, nyuma ya Mbeya City yenye pointi 46.

Loga amesema lazima ufanyike usajili mkubwa msimu ujao ili kuwa na kikosi bora katika nafasi zote kwa kusajili wachezaji wenye hadhi ya kuichezea Simba ambao wataleta ushindani.

“Simba inahitaji marekebisho makubwa katika nafasi zote kuanzia kipa hadi washambuliaji, wachezaji wanaotakiwa kusajiliwa wawe na hadhi pamoja na viwango vya kuweza kuichezea Simba na si kama ilivyo sasa wachezaji wengi siyo wazuri.
“Sijajua mchezaji gani anafaa lakini wanatakiwa kusajili sehemu yoyote watakapoona kuna mchezaji anayefaa ili kuwa na kikosi bora.
“Bado uongozi unatafuta wachezaji kutoka sehemu mbalimbali,” alisema Loga.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic