April 21, 2014



 
SAID AKIMKABIDHI KOCHA OMOG JEZI YA AZAM WAKATI ALIPOTUA NA KUANZA KUINOA
Mwenyekiwa Klabu ya Azam FC, Said Mohammed, amerusha kombora kwa wanachama na mashabiki wa Yanga ambao wamezidi kuiandama Azam kuwa imenunua ubingwa.

Katika mechi za mwishoni kabla ya kumalizika kwa ligi, Azam imekuwa ikishutumiwa kutumia njia za mkato kwa kile kilichodaiwa na mashabiki wanaosadikika kuwa wa Yanga kwamba wanatoa hongo ili watwae ubingwa.

Said amesema anawafananisha Yanga na kioo kwa mantiki kwamba kama kweli Azam walihujumu basi nao ubingwa wowote ambao wamekuwa wakitwaa walikuwa wakihujumu.
“Tuhuma hizo nazifananisha na kioo. Kioo ukikitazama lazima ujiangalie mwenyewe. Kwa hiyo linalosemwa kama kweli wana uhakika kuwa tumekuwa tukihonga timu ili ziachie pointi, basi na sisi tuamini ndiyo imekuwa njia yao ya ubingwa,” alisema bosi huyo.
Azam walitwaa ubingwa wa msimu wa 2013/14 kwa rekodi ya kutopoteza mchezo wowote kama walivyofanya Simba mwaka 2009.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic