April 7, 2014




Na Saleh Ally
MANCHESTER United ndiyo ilikuwa timu inayosifika kwa kuwa na nafasi ya kupata mikwaju mingi ya penalti katika kipindi cha ndani ya dakika 90.

Kikosi hicho wakati kipo chini ya Alex Chapman Ferguson, kilikuwa kina sifa ya kuwa na ubora, fowadi kali lakini walikuwa wakifanikiwa kupata penalti nyingi ndani ya dakika 90.
Hali hiyo ya kupata penalti nyingi ilikuwa ikifanya watu wengi kulaumu kuhusiana na Man United kwamba imekuwa ikipata pointi nyingi kupitia mikwaju ya penalti.
Lakini sasa mambo yanaonekana yamehamia Anfield kwa kuwa Liverpool ndiyo timu inayoongoza kwa kupata mikwaju mingi ya penalti.
Kabla ya mechi ya jana dhidi ya West Ham, Liverpool ilikuwa inaongoza kwa kupata mikwaju nane ya penalti iliyokuwa imetumbukizwa wavuni.
Idadi hiyo ni zaidi takribani asilimia 11 ya mabao yake 89 iliyoyafunga katika mechi zake 33 za ligi hiyo. Kwa kuwa katika mechi ya jana dhidi ya West Ham, Liverpool walipata penalti nyingine mbili.

Kasi ya ufungaji ya washambuliaji wake wawili, Luis Suarez mwenye mabao 29 na Daniel Sturridge mwenye 20, maarufu kama SAS iko juu sana.
Lakini wadau wa soka wamemlaumu Suarez kwamba amekuwa anaongoza kujiangusha, kitu ambacho ni sawa na ulaghai ambao unaiongezea Liverpool rundo la mikwaju ya penalti.
Liverpool imefunga penalti hizo kumi na  kufungwa mbili tu, hivyo kuwa timu iliyopewa mikwaju mingi zaidi na waamuzi wakati ligi hiyo ikiwa inaenda ukingoni.
Man City inafuatia baada ya kupata penalti sita, huku ikiwa imefungwa mkwaju mmoja tu wa penalti. Chelsea inashika nafasi ya tatu kwa kuwa na mikwaju mitano wakati haijawahi kufungwa hata mkwaju mmoja.
Manchester United iliyokuwa kinara, sasa ina mikwaju minne tu iliyofunga huku ikiwa imefungwa penalti mbili. Maana yake ni, ina nusu ya ile ya Liverpool.
Crystal Palace, Sunderland na Tottehham Hotspur kila moja pia imepata mikwaju hiyo minne kama ya Man United ambayo inaiondoa timu hiyo kwenye kundi la timu zinazopata penalti nyingi sana kwa msimu.
Ila Palace pamoja na kupata penalti nne, ina rekodi mbaya kwani imefungwa penalti sita ukilinganisha na Spurs iliyofungwa tatu na Sunderland mbili.
Hata hivyo, mshambuliaji nyota wa zamani wa Liverpool, Michael Owen, amesema mara nyingi fowadi yenye washambuliaji wakali na wasumbufu ndiyo yenye nafasi ya kupata penalti nyingi.
Wakati akifanya uchambuzi wa Premiership kwenye runinga ya Sky Sports, Owen amesema kama timu inashambulia sana na ina washambuliaji wenye kasi na uchu wa mabao, uwezekano wa kupata rundo la penalti ni kawaida.

Fin.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic