April 7, 2014





Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya umefanikiwa kuwa wa pili katika viwanja vinavyotumiwa na timu za ligi kuu kwa kuweza kuingiza mapato mengi katika mzunguko huu wa pili wa Ligi Kuu Bara.


Mpaka sasa, uwanja huo umeingiza kiasi cha Sh 195, 454, 000.00 ambazo ni sawa na asilimia 15.98.
Sokoine, katika msimu huu kwa mara ya kwanza imekuwa ikitumiwa na timu mbili ambazo ni wawakilishi wa mkoa huo, Tanzania Prisons na Mbeya City na kwa mara ya kwanza imeingiza kiasi kikubwa namna hiyo, ikiwa ni baada ya Mbeya City kupanda daraja.
Katika viwanja vyote, Uwanja wa Taifa wa Dar es Salaam, ndiyo wa kwanza na siku zote huwa unafanya vyema lakini Sokoine umeanza kuleta changamoto kutokana na kufanya vizuri kwa timu ya Mbeya City.

Uwanja wa Sheikh Amri Abeid wa Arusha ni wa mwisho, ukiwa umeingiza Sh milioni 1,890,000.00 katika mzunguko wa pili, sawa na asilimia 0.15. Uwanja huo hutumiwa na JKT Oljoro pekee.

Uwanja wa Chamazi, unaotumiwa na vinara wa ligi, Azam pamoja na Ashanti United na JKT Ruvu, wenyewe umeingiza Sh 17,166,000.00 ukishika nafasi ya sita.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic