April 7, 2014





Mshambuliaji wa kimataifa wa Simba, Mrundi, Amissi Tambwe, amewataka viongozi wa klabu hiyo kutafakari mara mia maombi yake ya kumwongezea maslahi na kama wakipuuza, basi yeye ataondoka na kwenda kujiunga na timu nyingine ambazo zinamhi.


Tambwe amesema anataka mshahara kama anaolipwa kiungo mshambuliaji wa Yanga, Emmanuel Okwi.

Okwi analipwa na Yanga kwa mwezi dola 4,000, zaidi ya Sh milioni 6, wakati Tambwe analipwa na Simba dola 1,000, zaidi ya Sh milioni 1.6.

Hali hiyo imekuwa ikimuumiza kichwa mchezaji huyo na kuutaka uongozi wa Simba kumwongezea maslahi kama anayopewa Okwi na Yanga kwa sababu kiwango chake ni 
bora zaidi ya mshambuliaji huyo raia wa Uganda. 

Tambwe amesema kuwa yeye amekuja Tanzania kutafuta fedha, hakuja kuuza sura, hivyo ameutaka uongozi wa Simba kumwongezea maslahi ili aweze kuendelea kuitumikia klabu hiyo iliyomsajili akitokea Vital’O ya Burundi.
Alisema endapo uongozi huo utapuuza maombi yake hayo, basi ataondoka na kwenda kujiunga na timu nyingine ambazo alidai kuwa anaendelea kufanya nazo mazungumzo kupitia kwa wakala wake ambaye sasa yupo jijini Dar es Salaam.
“Simba naipenda sana lakini wasipotaka kusikiliza maombi yangu niliyowaambia basi mimi nitaondoka na sisemi haya kwa kutania.
“Nimekuja Tanzania kutafuta pesa, sikuja kuuza sura, nachotaka ni maslahi mazuri ili niendelee kuitumikia Simba, kama wasipofanya hivyo nitaondoka zangu na wala siogopi kwani timu hiyo siyo ya baba yangu,” alisema Tambwe ambaye anaongoza kwa kuzifumania nyavu, akiwa na mabao 19.
Hata hivyo, uongozi wa Simba kupitia kwa katibu wake mkuu, Ezekiel Kamwaga umemtaka Tambwe kutulia na kufanya kazi yake.
“Tambwe anatakiwa kutulia na kufanya kazi yake, kwani tumeshajua ni jambo gani ambalo anahitaji, taratibu zipo hivyo inabidi azifuate na siyo kuongea katika vyombo vya habari,” alisema Kamwaga.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic