April 19, 2014



Mashabiki wamezidi kuonyesha kuzidiwa na mapenzi kila inapochezwa mechi ya watani Yanga na Simba.

Baadhi ya mashabiki wamezimia leo baada ya Simba kupata bao katika dakika ya 82, wakabebwa na kupatiwa huduma ya kwanza.
Dakika chache baadaye Simon Msuva akaisawazishia Yanga, ilikuwa katika dakika ya 85.
Baada ya hapo, mashabiki wengine wa Yanga walioshituka kwa furaha na wale wa Simba, waliotishwa na bao hilo, wakazimia pia.
Watu wa msalaba mwekundu wakaanza kufanya kazi ya ziada kuhakikisha wanawapa huduma.

Timu hizo zilimaliza mechi hiyo kwa sare ya mabao 1-1 na kumaliza ubishi kuwa nani ni zaidi ya mwenzake.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic