April 30, 2014



Muuaji wa bao la tatu kwenye mchezo wa kirafiki kati ya Taifa Stars na Burundi ‘Intamba Murugamba’, Yusuf Ndikumana, ana asili ya Tanzania.

Jumamosi ya wiki iliyopita kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar, timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, ilishindwa kufurukuta baada ya kukubali kipigo cha mabao 3-0, huku bao la tatu likifungwa kwa umbali wa mita 50 na kiungo wa timu hiyo, Ndikumana.
Ndikumana amesema kuwa bao alilofunga amemzawadia baba yake mzazi, Shekhe Songoro Mustafa, ambaye ni Mtanzania anayeishi hapa nchini.
“Najisikia raha sana kufunga bao kama lile ambalo nalipeleka kwa baba yangu Shekhe Songoro Mustafa, ambaye ni Mtanzania ila alikuja Burundi kikazi miaka ya nyuma na kunizaa baada ya kumuoa mama yangu ambaye ni raia wa Burundi.
“Bao lile ni la kwake kwa sababu yeye ndiye mtu aliyeniambia nikiingia katika mchezo ule nitulie ili niweze kufunga kwani riziki huwa zinakuja kwenye nafasi na hata nilipokuwa na mpira nilimuona kipa amesogea kwa mbele ndipo nikaupiga na kuingia moja kwa moja wavuni,” alisema Ndikumana.
Ndikumana anacheza katika Klabu ya Lydia Ludic Burundi Academie inayoongoza ligi ya nchi hiyo huku ikibakiwa na michezo nane kumaliza ligi hiyo.

   

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic