April 18, 2014


Baada ya Rhino Rangers na JKT Oljoro kupunga mkono wa kwa heri Ligi Kuu Bara, sasa imebakia nafasi moja kati ya Tanzania Prisons ya Mbeya, Ashanti ya Dar au Mgambo ya Tanga, yoyote inaweza kushuka daraja.


Prisons na Ashanti zinatarajia kukipiga kesho Jumamosi kwenye mechi ya mwisho ya Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro ambapo timu zote zina pointi 25, lakini sare au kufungwa kwa Ashanti kutamaanisha kuwa timu hiyo nayo rasmi imeshuka daraja.

Prisons inahitaji sare yoyote au ushindi ili ibaki ligi kuu, wakati Ashanti inahitaji ushindi wowote ili ijihakikishie kubaki, Mgambo ambayo inacheza dhidi ya Mbeya City ikifungwa kwa tofauti ya mabao mawili huku Ashanti na Prisons zikipata sare, maana yake ni kuwa Mgambo itashuka kwa kuzingatia tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa.

Nahodha wa Ashanti, Abuu Mtiro amesema wamepata nguvu baada ya kuifunga Simba na wanaenda kupambana na Prisons kwa nguvu zote. “Mchezo wa Jumamosi utakuwa mgumu kwa sababu wote tuna pointi sawa, hivyo tunahitaji ushindi ili tuweze kubaki ligi kuu.

“Ushindi tulioupata dhidi ya Simba ndiyo umetupa matumaini kupata nafasi ya kubaki na tutajitahidi kuhakikisha msimu ujao tunashiriki tena ligi kuu,” alisema Mtiro. 

Msimamo ulivyo
 P      GD    Pts
10. Mgambo    25     -16   26    
11. Prisons      25     -8      25    
12. Ashanti       25     -18   25    
13. Oljoro        25     -18   18    

14. Rhino         25     -19   16     

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic