June 27, 2014




Juhudi za kutaka kuzuia uchaguzi kwa kundi la wanachama wachache zimekwama na sasa uchaguzi huo mkuu wa Simba utafanyika Jumapili kama ulivyopangwa.
Mahakama Kuu imeamua uchaguzi utafanyika vilevile kama ulivyopangwa baada ya kusikiliza kesi iliyokuwa na mvutano mkubwa.
Uamuzi huo umetolewa leo na Jaji Augustine Mwarija ambaye alisema mahakama inakubali wanachama kufungua kesi lakini inakataa kuzuia uchaguzi wa Simba kwa sababu hakukuwa na kesi ya msingi ya madai.
Jaji Mwarija alisisitiza hivyo ombi la zuio lililetwa kabla ya muda.
Lakini ajabu, wakili Mwenyekiti wa Rais wa Simba, Aden Rage na wenzake wa bodi ya wadhamini, Juma Nassoro alionyesha kusikitishwa na uchaguzi kutosimamishwa.
 “Uongozi wa Simba ndiyo ulikuwa na mamlaka ya kutaka uchaguzi uendelee au la,” alisema Nassoro na kuwashangaza wengi.
Baadhi ya wanachama waliokuwa katika eneo hilo walionyesha kushangazwa na kusema inawezekana mwenyekiti huyo anayemaliza muda wake alikuwa anapigia chepuo uchaguzi usimamishwe.
“Sasa Rage angefaidika na nini kama alitaka uchaguzi usimamishwe, nimeshangazwa na maneno ya wakili wake.
“Hiki si kitu kizuri, lazima watu waangalie maslahi ya Simba na si vinginevyo,” alisema Juma Mshamu ambaye alisema ni mwanachama kutoka Morogoro.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic