June 28, 2014



WINGA wa zamani wa timu za Yanga na Simba, Said Maulid ‘SMG’, wiki iliyopita alimwaga wino wa kuitumikia Onze Bravos Dos Maquis ya Angola kwa mkataba wa mwaka mmoja wenye thamani ya shilingi milioni 15.

SMG aliondoka nchini na kuelekea Angola, wiki mbili zilizopita kwa ajili ya kukamilisha taratibu za kuichezea baada ya kufanya mawasiliano ya siku chache baina yake na uongozi wa Onze Bravos.
Rafiki wa karibu na mchezaji huyo amesema kwa kuwa  SMG alishamalizana na uongozi kabla ya kuondoka nchini, alipofika Angola zoezi lililobaki lilikuwa ni kumwaga wino, ambalo limekamilika wiki iliyopita na kukabidhiwa milioni zake hizo.
Aliongeza kuwa walikubaliana mambo kadhaa ikiwemo kuwa anaweza kuongezewa mkataba kwa ajili ya msimu ujao kutokana na maendeleo yake klabuni hapo huku dili la kwenda kuchukua mafunzo ya ukocha nchi za Ureno na Brazil likiwa palepale baada ya kutimiza  miaka minne akiitumikia timu hiyo iliyomaliza nafasi ya sita msimu uliopita.
“Wamempa zaidi ya milioni 15 kama ada yake ya usajili na mkataba wa mwaka  mmoja, lile dili lao lipo palepale la kwenda kwenye mafunzo ya ukocha kati ya Brazil na Ureno lakini pia wamekubaliana kuwa wanaweza kumuongezea mkataba kutokana na ‘performance’ yake,” alisema mtoa taarifa huyo.
SMG alitua Onze Bravos kwa mara ya kwanza mwaka 2008 akitokea Yanga na kisha kurejea msimu uliopita kukipiga Ashanti iliyoshuka daraja.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic