June 28, 2014

DALALI (KULIA) AKIWA NA EVANS AVEVA


Mwenyekiti wa zamani wa Klabu ya Simba, Hassan Dalali, amewashukia wanachama ambao wamekuwa wakilalamikia vitendo vya usajili vinavyofanywa kwenye klabu hiyo kwa kuwaambia wengi wao hawajui ugumu wa kazi hiyo, lakini kama wanataka kufanya hivyo basi wasajili wao.


Usajili wa Simba upo chini ya mwenyekiti wao, Zacharia Hans Pope ambapo mpaka sasa tayari wameshafanikiwa kupata saini za wachezaji Joram Nasson na Mohammed Hussein ‘Tshabalala’.

Akizungumza na Championi Jumamosi, Dalali alisema wanachama hao hawajajua ni ugumu gani ambao wanaupata kwenye usajili wa wachezaji, hivyo wanatakiwa wasipewe lawama zozote na kama watataka kusajili wachezaji wao basi wafanye hivyo.
“Utakuta kiongozi unapewa lawama kisa mchezaji fulani imeshindikana kusajiliwa, lakini watu hao bado hawajui ni ugumu gani ambao tunakutana nao kwenye usajili huo, lakini kama watataka kudhibitisha hivyo nawaambia wajaribu kusajili mchezaji mmoja ili nao waone,” alisema Dalali.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic