July 2, 2014



Mshambuliaji wa Yanga, Jerry Tegete, amepewa kibarua na kocha mkuu wa timu hiyo Mbrazili, Marcio Maximo, cha kuwa mkalimani kwa wachezaji wenzake.
Kazi hiyo aliianza jana asubuhi kwenye Ufukwe wa Coco, Oysterbay jijini Dar es Salaam, ikiwa ni siku ya kwanza kocha wa timu hiyo kuanza mazoezi ya pamoja na kikosi hicho.
Wakati mazoezi hayo yakiendelea, kocha huyo na msaidizi wake, Leonardo Neiva, walionekana wakimtumia mshambuliaji huyo kuwatafsiria wachezaji wenzake kile walichokuwa wakisema.
Makocha hao wakiwa wanaendelea na programu zao, walikuwa wakitumia Lugha ya Kiingereza na baadaye mshambuliaji huyo kuwatafsiria wachezaji wenzake kwa Kiswahili.
Mshambuliaji huyo alilazimika kuwatafsiria wachezaji wenzake kwa kila programu ya mazoezi iliyokuwa inabadilishwa na makocha.
Mazoezi waliyokuwa wanayafanya ni kukimbia mbio fupi na ndefu mchangani huku wakimalizia kwa kuruka koni.
Akizungumzia hali hiyo, Tegete alisema: “Siyo mara ya kwanza kunipa kazi hiyo ya kuwatafsiria wachezaji wenzagu, tangu akiwa anaifundisha Taifa Stars alikuwa ananitumia.
“Mimi nimeshazoea kwa sababu lugha hiyo ninaijua vizuri, hivyo sioni shida kwangu, ndiyo maana muda mwingi walikuwa wakiita na kunipa maelekezo na baadaye kuwaelezea wenzangu.”

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic