July 2, 2014



Baada ya uongozi mpya wa Simba kuingia madarakani, mshambuliaji Mrundi Amissi Tambwe, amefunguka kuwa hatarejea klabuni hapo hadi watakapokaa na kujadiliana tena kuhusiana na maslahi yake.


Tambwe ambaye msimu uliopita aliibuka mfungaji bora baada ya kufunga mabao 19, amesema hawezi kurudi kwenye timu hiyo hata kama ina uongozi mpya mpaka atakapotimiziwa mahitaji yake.

Simba ilifanya uchaguzi wake wikiendi iliyopita na kufanikiwa kuwaweka madarakani Evans Aveva kama rais na Geofrey Nyange ‘Kaburu’ kama makamu wake.

Awali, klabu hiyo ilimuahidi mshambuliaji huyo kuwa atakaporejea msimu ujao itaboresha mkataba wake, ingawa anasema kuwa hakuna chochote ambacho kimefanyika hadi sasa.

Akizungumza kutoka Bujurumbura, Burundi, straika huyo alisema klabu yake inahitaji kumtimizia mahitaji yake mapema kama walivyokuwa wamekubaliana na kwa kuboreshewa mkataba, usafiri na vitu vya ndani ndiyo aweze kuja nchini.

“Kikubwa kwa sasa nahitaji kuboreshewa maslahi yangu kuanzia mkataba wenyewe na hata mazingira ninayoishi na usafiri pia,  ili niweze kufurahia matunda ya kazi yangu.

“Hili suala waliniahidi wenyewe, ndiyo maana wanatakiwa kunitimizia mapema kabla hata ligi haijaanza ili kuweza kujipanga mapema maana tunakoelekea changamoto ni wazi zitakuwa kubwa katika ligi yetu.

Ukweli siwezi kurejea kwa sasa mpaka nitapofahamu kuwa mambo hayo yapo vizuri,” alisema Tambwe ambaye amekuwa akiwindwa na timu kadhaa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic