July 6, 2014




Mshambuliaji nyota wa Brazil, Neymar amesema wenzake bado wana nafasi kubwa ya kumsaidia kutimiza ndoto yake ya kutwaa Kombe la Dunia.
Huku akimwaga machozi, Neymar amesema kuumia kwake hakuwezi kuwa mwisho wa ndoto zake na Brazil kutwaa Kombe la Dunia.

Nafasi ipo, ninawaamini wenzangu wanaweza kufanya jambo na kutimiza ndoto.
Mimi nilikuwa ni sehemu ya timu, hivyo bado timu ina uwezo wa kutimiza malengo yetu.
Nawatakia wenzangu wote kila la kheri ili wafikie ndoto zetu, alisema.
Neymar aliumizwa na beki wa Colombia katika mechi ya robo fainali.
Beki huyo amemvunja mfupa mdogo wa uti wa mgongo, hali inayosababisha aikose michuano hiyo hadi mwisho.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic