July 29, 2014



Kocha Hans van der Pluijm amesikitisha kutokana na kitendo cha klabu ya Shaolla FC ya Saudi Arabia kuvunja mkataba wao kienyeji.

Pluijm raia wa Uholanzi na msaidizi wake, Charles Boniface Mkwasa hawataendelea kuifundisha timu hiyo baada ya uongozi wa klabu kuvunja mkataba wao.
Mkataba umevunjwa na tayari wawili hao ambao kwa pamoja waliinoa Yanga wako katika hatua za mwisho kurejea Ghana na Tanzania.
“Ni kitu cha kusikitisha sana, kwa wiki tatu tulizofanya kazi hapa tulikuwa tumeleta mabadiliko makubwa sana na wachezaji walikuwa na furaha na sisi.

“Kuna wale ambao walikuwa hawana nafasi katika kikosi cha kocha aliyepita, lakini tayari walionyesha mabadiliko makubwa.

“Tulikuwa tunategemea kuwa na kikosi kizuri baada ya kuanza kwa ligi, lakini mambo yakaharibika baada ya viongozi mbalimbalia kuanza kuleta wachezaji wao,” alisema Pluijm wakati akihojiwa na SALEHJEMBE.

“Tuliwafanyia majaribio wachezaji hao na kuona walikuwa na viwango duni, tukawakataa. Hilo liliwaudhi sana viongozi.

“Baada ya siku chache wakatangaza kuvunja mkataba, imetushangaza sana. Niseme wazi nimesikitishwa na hilo.”
Pluijm ndiye alikuwa wa kwanza kupata kazi katika klabu hiyo, naye akampigia ‘pande’ Charles Boniface Mkwasa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic