July 7, 2014



Uongozi wa Simba uko kwenye mjadala wa kuamua timu yao iweke wapi kambi fupi kabla ya kuanza msimu mpya wa 2014-15.


Afrika Kusini na Oman ndiyo sehemu zinazotajwa kwa ajili ya kambi hiyo, lakini kuna mambo mawili.
Oman kuna joto kali sana ambalo wakati mwingine hufikia hadi nyuzi joto 40 na ushee, hivyo Simba watalazimika kufanya mazoezi usiku tu joto linaposhuka.

Afrika Kusini ni baridi kali kipindi hiki, wakati mwingine inakwenda hadi nyuzijoto 2. Hivyo Simba watakuwa katika wakati mgumu na watalazimika kufanya mazoezi mchana tu kwa kuwa asubuhi sana au usiku, joto ni kali sana.

Hivyo Simba wako kwenye mjadala sehemu ya kwenda ingawa timu hiyo itaanza mazoezi jijini Dar es Salaam kabla ya kufunga safari kwenda Zanzibar.

Baada ya Zanzibar, Simba itaanza safari kati ya Afrika Kusini au Oman kutokana na watakachokuwa wamefikia.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic