August 30, 2014

 West Ham imefanya kweli baada ya leo kumtangaza kiungo mkabaji wa Barcelona, Alex Song ni mali yao.
Song amewasalimia mashabiki wa West Ham mara tu baada ya kutua London na kusaini mkataba wa mkopo wa muda mrefu na klabu hiyo.

Mcameroon huyo mwenye umri wa miaka 26 alihaha kupata nafasi ya kudumu katika kikosi cha kwanza cha Catalan.
Aliondoka Arsenal mwaka 2012 kwenda Camp Nou lakini ameamua kurejea tena kwenye Barclays Premier na kujiunga na Wagonga nyundo hao wa London.
West Ham imeshinda vita ya kumpata baada ya klabu kadhaa kama Napoli ya Italia na Galatasaray ya Uturuki nazo kuonyesha nia ya kumpata.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic