Kweli Kocha Louis van Gaal ameanza na mguu mbaya maana Man United imefungwa mabao 2-1 na Swansea, lakini kibaya zaidi ni kupoteza mechi ya kwanza ya ligi.
Man
United ilikuwa haijapoteza mechi ya ugenini tokea mwaka 1972, lakini mzigo wa
kuivuruga rekodi hiyo umeangukia van Gaal.
Hata
David Moyes ambaye aliboronga msimu uliopita, alijitahidi na kushinda mechi ya
kwanza ya msimu.
Baadhi
ya mashabiki wa Man United wameonyesha hawana subira na kusema van Gaal
amewakera.
Lakini
Mholanzi huyo amejibu kwa kusema kikosi chake hakikucheza kitimu na yeye ndiye
anawajibika.
0 COMMENTS:
Post a Comment