August 30, 2014



Msimu mpya unaanza mwezi ujao, tayari makocha wameanza kujua vikosi vyao vya kwanza, kipa Deogratius Munishi ‘Dida’ ametajwa kuwa ndiye atakuwa chaguo la kwanza katika kikosi cha Yanga, ikiwa na maana kwamba amewapiga bao Juma Kaseja na Ally Mustapha ‘Barthez’.


Kocha Mkuu wa Yanga, Marcio Maximo, ametamka wazi kuwa kipa huyo ndiye atakaye kuwa changuo la kwanza, kutokana na kuwa na uwezo hasa ikizingatiwa ndiye chaguo la kwanza katika timu ya taifa,Taifa Stars.

Maximo ameliambia gazeti hili, kuwa hawezi kuzungumzia uwezo wa mchezaji mmoja-mmoja lakini kwa upande wa kikosi chake bado Dida atakuwa namba moja.

“Kwa sasa naweza kusema kipa namba moja ni Dida, kutokana na kuwa na kiwango bora, ndiyo maana hata timu ya taifa wamemuamini na wamekuwa wakimtumia mara kwa mara lakini klabu itategemeana na uwezo ambao atakaounyesha,” alisema Maximo.
Alikwenda mbali na kusema kuwa tayari kwake amewapanga ambapo Juma Kaseja ni chaguo la pili huku Barthez akiwa wa tatu, japo amesema wote wanaelekeana viwango.

Ikumbukwe katika msimu uliopita katika mzunguko wa pili Dida alidaka takribani michezo yote na Barthez aliweza kusugua benchi mpaka msimu ulipomalizika.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic