FIGO KATIKATI YA SHABANI RAMADHANI NA NSAJIGWA |
Kikosi
cha wakongwe wa Real Madrid kimewaonyesha soka wakongwe wa Tanzania kwa
kuwachapa mabao 3-1.
Katika
mechi hiyo iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam na
kuhudhuriwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Jakaya Kikwete.
Mabao
ya Real Madrid, yote matatu yalifungwa na Ruben de la Red ambaye alianza
kufunga moja katika kipindi cha kwanza.
Lakini
Tanzania Eleven wakasawazisha baada ya Roberto Rojas kujifunga wakati akijaribu
kuokoa.
Kipindi
cha pili, De la Red akafunga mengine mawili, moja likiwa la mkwaju wa penalty.
Luis
Figo ndiye alikuwa kivutio zaidi kwa mashabiki wengi waliojitokeza kwenye
uwanja huo.
Mashabiki
wengi walikuwa wakimshangilia wakati akiwahenyesha mabeki Shadrack Nsajigwa,
Mecky Maxime na Salum Sued.
Madrid
ndiyo walikuwa kivutio zaidi kutokana na kucheza kwa kuonana zaidi.
Pasi
zao zilikuwa za uhakika kuliko kikosi hicho chini ya Boniface Mkwasa na Jamhuri
Kihwelo ‘Julio’.
DE LA RED AKIKABWA NA ATHUMANI CHINA NA HABIB KONDO |
Hata
hivyo, safu ya ushambuliaji ya Tanzania Eleven iliyoongozwa na Madaraka Selemani
na Kali Ongala ilionekana kutokuwa na makali sana.
Ongala,
Sabri Ramadhani ‘China’ na Athumani ‘China’ ndiyo walionyesha uhai zaidi
katikati.
Lakini
bado wasingeweza wenyewe hivyo kufanya kuwe na ugumu.
Mwisho,
Rais Kikwete aliwakabidhi kombe Madrid ikiwa ni ishara ya kushinda mechi hiyo
iliyoandaliwa na kampuni ya TSN na kudhaminiwa na makampuni kadhaa kama
Sapphire Court Hotel, Fast Jet, Bin Slum Tyres, Championi na TSN yenyewe.
Ahaa ni matokeo tu lazima shindi apatikane ila tujipange siku tukienda huko kwao tuwachape 6 kwa nunge
ReplyDelete