September 3, 2014

NDANDA SIKU ALIVYOINGIA MKATABA NA NDANDA FC

Baada ya Ndanda FC kupata nafasi ya kushiriki Ligi Kuu Bara, mashabiki wa timu hiyo wamejipanga kuhakikisha timu yao inaibuka na ushindi katika mechi zao mbili za mwanzo.

Ndanda inayodhaminiwa na Bin Slum Tyres Ltd inatarajiwa kufungua Dimba Septemba 20, kwa kucheza na Stand United kwenye Uwanja wa Kambarage na baadaye itasafiri mpaka Morogoro kupambana na Mtibwa Sugar.
Mdau wa timu hiyo na pia meneja wa Uwanja wa Nangwanda Sijaona, John Mapunda, alisema mashabiki hao wamejipanga kikamilifu kuhakikisha timu yao inakusanya pointi sita za mwanzo ambapo watacheza ugenini.
“Tayari mashabiki wameshaanza kupanga mipango ya kuhakikisha Ndanda inapata pointi sita za mwanzo ambazo ni muhimu ukizingatia itakuwa inacheza ugenini.

“Katika kuhakikisha wanapata pointi hizo, wamedhamiria kusafiri na timu yao popote itakapokwenda ili wakatoe sapoti ya nguvu,” alisema Mapunda.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic