September 3, 2014

Mshambuliaji wa kimataifa wa Yanga, Mbrazil, Genilson 

Santos ‘Jaja’, ndiye atakayehusika na penalti zote za klabu hiyo zitakazotokea katika mechi baada ya kumkosha kocha mkuu, Marcio Maximo kwa uwezo wake wa kupiga mipira hiyo.
Jaja ambaye ametua nchini kuitumikia Yanga akitokea Brazil, anasifika pia kwa uwezo mkubwa wa kucheza mipira ya vichwa, umaliziaji wa krosi na kupiga mashuti yanayolenga goli.
Katika mazoezi ya timu hiyo yanayofanyika katika Uwanja wa Shule ya Sekondari Loyola jijini Dar, Maximo aliwateua wapiga penalti watatu, Said Bahanuzi, Simon Msuva na Jaja na kuwapa zoezi maalum la kupiga penalti dhidi ya makipa, Juma Kaseja na Ally Mustapha ‘Barthez’.
Jaja ndiye aliyeibuka kinara wa matuta baada ya kupiga penalti kumi na kufunga tisa huku moja ikigonga mtambaa wa panya. Bahanuzi naye alionyesha umahiri baada ya kufunga nane kati ya kumi huku Kaseja na Barthez kila mmoja akidaka tuta mojamoja. Msuva alifunga sita kati ya kumi na kukosa nyingine ambazo zilipaa na kudakwa na makipa.
Maximo ambaye alikuwa pembeni akishuhudia zoezi hilo, alionyesha kufurahia uwezo mkubwa wa Jaja katika upigaji wa penalty, jambo linalodhihirisha kuwa katika mechi kama itatokea penalti basi chaguo la Maximo kuipiga ni Jaja.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic